Monday, October 31, 2016

YANGA mabingwa watetezi Tanzania bara



Image result for Bossou akishangilia goli

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu soka Tanzania bara klabu ya  Young Africans wamerudi dimbani kucheza mchezo wao 12 wa Ligi Kuu sokaTanzania bara msimu wa 2016/2017 wakiongozwa na kocha wao Hans van Pluijm baada ya kufuta mawazo ya kujiuzulu.


Timu ya Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 3-0, magoli yaliyofungwa na bekiVincent Bossou, dakika ya 49 na goli kipa wa Mbao FC Emmanuel Mseja akijifunga kwa kushindwa kuzuia mpira uliorushwa na  Mbuyu Twite dakika ya 56, Amissi Tambwe  alikamilisha  idadi magoli mnamo dakika ya 75 na kukamilisha jumla ya magoli 3-0.      


chanzo: manchorypascal.blogspot.com  

No comments:

Post a Comment